HEAVEN GLORY CHAPTER
"Kwaya ya Kanisa Iliyoungana katika mapambano Dhidi ya Matumizi ya Dawa za Kulevya"
Sisi ni Nani
Heaven Glory Chapter ni tawi la Mtandao wa Kuzuia Matumizi ya Dawa za Kulevya Tanzania (TDPN), ikiwa ni juhudi za kidini zinazolenga kupambana na matumizi ya dawa za kulevya kupitia mwongozo wa kiroho, elimu, na msaada wa kijamii. Kama kwaya ya kanisa, tunaunganisha sauti zetu si tu kwa ibada bali pia kwa utetezi, tukiwaelimisha watu juu ya madhara ya dawa za kulevya na kutoa msaada kwa wale walioathirika na uraibu.
Tunachofanya
Tunajihusisha na jamii kwa njia zifuatazo:
- Kuongeza Uelewa – Kuendesha kampeni za elimu kuhusu hathari za matumizi ya dawa za kulevya.
- Kusaidia Urejeo – Kutoa msaada wa kiroho na kihisia kwa wale wanaopambana kuachana na uraibu.
- Kuhamasisha Vijana – Kuwahimiza kufanya maamuzi chanya kupitia muziki wa kwaya, ushauri, na shughuli za kijamii.
- Kushirikiana na Wadau – Kushirikiana na mashirika ya ndani, makanisa, na taasisi za serikali ili kuhamasisha jamii isiyo na dawa za kulevya.
Lengo Letu
Dhamira yetu ni kutumia nguvu ya imani na muziki wa kwaya kuleta matumaini, kuelimisha jamii, na kusaidia watu katika safari yao ya kuachana na dawa za kulevya. Tunaamini kuwa kupitia umoja, maombi, na kuchukua hatua sahihi na madhubuti, tunaweza kuleta mabadiliko ya kudumu katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.
Wasiliana Nasi
Tuko hapa kukusaidia na kushirikiana nawe. Wasiliana nasi ili kushiriki au kupata msaada: